Rukia maudhui

circa 1446 BC

Moses & The Exodus

God raises up Moses to confront Pharaoh; the ten plagues culminate in Israel's dramatic deliverance from four centuries of bondage.

415 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Kutoka 6:3takriban 1491 KK

    Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.

  2. Kutoka 6:4takriban 1491 KK

    Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.

  3. Kutoka 6:5takriban 1491 KK

    Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.

  4. Kutoka 6:6takriban 1491 KK

    “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.

  5. Kutoka 6:7takriban 1491 KK

    Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.

  6. Kutoka 6:8takriban 1491 KK

    Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’ ”

  7. Kutoka 6:9takriban 1491 KK

    Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.

  8. Kutoka 6:10takriban 1491 KK

    Ndipo Bwana akamwambia Mose,

  9. Kutoka 6:11takriban 1491 KK

    “Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”

  10. Kutoka 6:12takriban 1491 KK

    Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”

  11. Kutoka 6:13takriban 1491 KK

    Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.

  12. Kutoka 6:14takriban 1491 KK

    Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.

  13. Kutoka 6:15takriban 1491 KK

    Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.

  14. Kutoka 6:16takriban 1491 KK

    Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.

  15. Kutoka 6:17takriban 1491 KK

    Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.

  16. Kutoka 6:18takriban 1491 KK

    Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.

  17. Kutoka 6:19takriban 1491 KK

    Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.

  18. Kutoka 6:20takriban 1491 KK

    Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.

  19. Kutoka 6:21takriban 1491 KK

    Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.

  20. Kutoka 6:22takriban 1491 KK

    Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.

  21. Kutoka 6:23takriban 1491 KK

    Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.

  22. Kutoka 6:24takriban 1491 KK

    Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.

  23. Kutoka 6:25takriban 1491 KK

    Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.

  24. Kutoka 6:26takriban 1491 KK

    Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”

  25. Kutoka 6:27takriban 1491 KK

    Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.