God
Mistari inayomtaja God
Ngurumo yako ilisikika katika upepo wa kisulisuli, umeme wako wa radi ukaangaza dunia, nchi ikatetemeka na kutikisika.
Njia yako ilipita baharini, mapito yako kwenye maji makuu, ingawa nyayo zako hazikuonekana.
Uliongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Mose na Aroni.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.