God
Mistari inayomtaja God
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?