- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi118
Listen to this chapter
0:00
0:00
Wito wa Kumshukuru Mungu Ulimwenguni
1
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2
Israeli na aseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
3
Nyumba ya Aroni na iseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
4
Wote wamchao Bwana na waseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
Ushuhuda wa Wokovu na Tumaini
5
Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, naye akanijibu kwa kuniweka huru.
6
Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
7
Bwana yuko pamoja nami, yeye ni msaidizi wangu. Nitawatazama adui zangu wakiwa wameshindwa.
8
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kumtumainia mwanadamu.
9
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wakuu.
10
Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
11
Walinizunguka pande zote, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
12
Walinizunguka kama kundi la nyuki, lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
13
Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, lakini Bwana alinisaidia.
14
Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, yeye amefanyika wokovu wangu.
Ushindi wa Nguvu za BWANA
15
Sauti za shangwe na ushindi zinavuma hemani mwa wenye haki: “Mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!
16
Mkono wa kuume wa Bwana umeinuliwa juu, mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!”
17
Sitakufa, bali nitaishi, nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda.
18
Bwana ameniadhibu vikali, lakini hakuniacha nife.
Kuingia Malangoni pa Wokovu
19
Nifungulie malango ya haki, nami nitaingia na kumshukuru Bwana.
20
Hili ni lango la Bwana ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
21
Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu, umekuwa wokovu wangu.
22
Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni.
23
Bwana ametenda hili, nalo ni la kushangaza machoni petu.
24
Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya, tushangilie na kufurahi ndani yake.
25
Ee Bwana, tuokoe, Ee Bwana, utujalie mafanikio.
26
Heri yule ajaye kwa jina la Bwana. Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki.
27
Bwana ndiye Mungu, naye ametuangazia nuru yake. Mkiwa na matawi mkononi, unganeni kwenye maandamano ya sikukuu hadi kwenye pembe za madhabahu.
Nadhiri ya Mwisho na Sifa
28
Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
29
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note