Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 4:7takriban 27 BK

    Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”

  2. Luka 4:8takriban 27 BK

    Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’ ”

  3. Luka 4:9takriban 27 BK

    Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,

  4. Luka 4:10takriban 27 BK

    kwa maana imeandikwa: “ ‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;

  5. Luka 4:11takriban 27 BK

    nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’ ”

  6. Luka 4:12takriban 27 BK

    Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”

  7. Luka 4:13takriban 27 BK

    Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.

  8. Luka 4:14takriban 27 BK

    Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.

  9. Luka 4:15takriban 27 BK

    Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.

  10. Luka 4:16takriban 27 BK

    Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,

  11. Luka 4:17takriban 27 BK

    naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:

  12. Luka 4:18takriban 27 BK

    “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,

  13. Luka 4:19takriban 27 BK

    na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”

  14. Luka 4:20takriban 27 BK

    Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.

  15. Luka 4:21takriban 27 BK

    Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”

  16. Luka 4:22takriban 27 BK

    Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”

  17. Luka 4:23takriban 27 BK

    Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’ ”

  18. Luka 4:24takriban 27 BK

    Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.

  19. Luka 4:25takriban 27 BK

    Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.

  20. Luka 4:26takriban 27 BK

    Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.

  21. Luka 4:27takriban 27 BK

    Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”

  22. Luka 4:28takriban 27 BK

    Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.

  23. Luka 4:29takriban 27 BK

    Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.

  24. Luka 4:30takriban 27 BK

    Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.

  25. Luka 4:31takriban 27 BK

    Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.