circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Luka 4:7takriban 27 BK
Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
- Luka 4:8takriban 27 BK
Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’ ”
- Luka 4:9takriban 27 BK
Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
- Luka 4:10takriban 27 BK
kwa maana imeandikwa: “ ‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
- Luka 4:11takriban 27 BK
nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’ ”
- Luka 4:12takriban 27 BK
Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”
- Luka 4:13takriban 27 BK
Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
- Luka 4:14takriban 27 BK
Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
- Luka 4:15takriban 27 BK
Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
- Luka 4:16takriban 27 BK
Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
- Luka 4:17takriban 27 BK
naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
- Luka 4:18takriban 27 BK
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
- Luka 4:19takriban 27 BK
na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
- Luka 4:20takriban 27 BK
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
- Luka 4:21takriban 27 BK
Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
- Luka 4:22takriban 27 BK
Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
- Luka 4:23takriban 27 BK
Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’ ”
- Luka 4:24takriban 27 BK
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
- Luka 4:25takriban 27 BK
Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
- Luka 4:26takriban 27 BK
Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
- Luka 4:27takriban 27 BK
Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
- Luka 4:28takriban 27 BK
Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
- Luka 4:29takriban 27 BK
Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
- Luka 4:30takriban 27 BK
Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
- Luka 4:31takriban 27 BK
Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.