Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Marko 3:32takriban 31 BK

    Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”

  2. Marko 3:33takriban 31 BK

    Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”

  3. Marko 3:34takriban 31 BK

    Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.

  4. Marko 3:35takriban 31 BK

    Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”

  5. Marko 4:1takriban 31 BK

    Yesu akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Umati wa watu uliokuwa umekusanyika kumzunguka ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba ilimbidi Yesu aingie kwenye mashua iliyokuwa baharini na kuketi humo, nao watu wote walikuwa ufuoni mwa bahari.

  6. Marko 4:2takriban 31 BK

    Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, naye katika mafundisho yake akasema:

  7. Marko 4:3takriban 31 BK

    “Sikilizeni! Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.

  8. Marko 4:4takriban 31 BK

    Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.

  9. Marko 4:5takriban 31 BK

    Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.

  10. Marko 4:6takriban 31 BK

    Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.

  11. Marko 4:7takriban 31 BK

    Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea, hivyo haikutoa mazao.

  12. Marko 4:8takriban 31 BK

    Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri, zikaota vizuri na kukua, zikatoa mazao, moja mara thelathini, nyingine mara sitini, na nyingine mara mia moja.”

  13. Marko 4:9takriban 31 BK

    Kisha Yesu akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”

  14. Marko 4:10takriban 31 BK

    Alipokuwa peke yake, watu waliokuwepo naye pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili wakamuuliza kuhusu mifano yake.

  15. Marko 4:11takriban 31 BK

    Naye akawaambia, “Ninyi mmepewa kujua siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kwa wale walioko nje, kila kitu husemwa kwao kwa mifano,

  16. Marko 4:12takriban 31 BK

    ili, “ ‘daima waone lakini wasitambue, daima wasikie lakini wasielewe; wasije wakageuka, wakatubu na kusamehewa!’ ”

  17. Marko 4:13takriban 31 BK

    Kisha Yesu akawauliza, “Hamwelewi maana ya mfano huu? Basi mtaelewaje mifano mingine?

  18. Marko 4:14takriban 31 BK

    Yule mpanzi hupanda neno.

  19. Marko 4:15takriban 31 BK

    Hawa ndio wale walio kando ya njia ambako neno lilipandwa. Walisikiapo neno, Shetani huja mara na kulinyakua lile neno lililopandwa ndani yao.

  20. Marko 4:16takriban 31 BK

    Nazo zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo wenye miamba, ni wale wanaolisikia neno, na mara hulipokea kwa furaha.

  21. Marko 4:17takriban 31 BK

    Lakini kwa kuwa hawana mizizi, wao hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, mara wao huiacha imani.

  22. Marko 4:18takriban 31 BK

    Lakini wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye miiba, hulisikia lile neno;

  23. Marko 4:19takriban 31 BK

    lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae.

  24. Marko 4:20takriban 31 BK

    Wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri, hulisikia lile neno, wakalipokea na kuzaa mazao. Wao huzaa mara thelathini, au mara sitini, au mara mia ya mbegu iliyopandwa.”

  25. Marko 4:21takriban 31 BK

    Akawaambia, “Je, taa huwashwa na kufunikwa chini ya kikapu au mvunguni mwa kitanda? Je, haiwashwi na kuwekwa juu ya kinara chake?