Rukia maudhui

circa 605–538 BC

The Babylonian Exile

Jerusalem falls and the temple burns; Ezekiel and Daniel minister among the exiles as Lamentations mourns the city's ruin.

1,784 mistari · 3 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Ezekieli 11:6takriban 594 KK

    Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.

  2. Ezekieli 11:7takriban 594 KK

    “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.

  3. Ezekieli 11:8takriban 594 KK

    Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.

  4. Ezekieli 11:9takriban 594 KK

    Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.

  5. Ezekieli 11:10takriban 594 KK

    Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.

  6. Ezekieli 11:11takriban 594 KK

    Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.

  7. Ezekieli 11:12takriban 594 KK

    Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”

  8. Ezekieli 11:13takriban 594 KK

    Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”

  9. Ezekieli 11:14takriban 594 KK

    Neno la Bwana likanijia kusema:

  10. Ezekieli 11:15takriban 594 KK

    “Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’

  11. Ezekieli 11:16takriban 594 KK

    “Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’

  12. Ezekieli 11:17takriban 594 KK

    “Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’

  13. Ezekieli 11:18takriban 594 KK

    “Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.

  14. Ezekieli 11:19takriban 594 KK

    Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.

  15. Ezekieli 11:20takriban 594 KK

    Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.

  16. Ezekieli 11:21takriban 594 KK

    Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”

  17. Ezekieli 11:22takriban 594 KK

    Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.

  18. Ezekieli 11:23takriban 594 KK

    Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.

  19. Ezekieli 11:24takriban 594 KK

    Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,

  20. Ezekieli 11:25takriban 594 KK

    nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.

  21. Ezekieli 12:1takriban 594 KK

    Neno la Bwana likanijia kusema:

  22. Ezekieli 12:2takriban 594 KK

    “Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.

  23. Ezekieli 12:3takriban 594 KK

    “Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi.

  24. Ezekieli 12:4takriban 594 KK

    Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni.

  25. Ezekieli 12:5takriban 594 KK

    Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.