God
Mistari inayomtaja God
lakini hakika Mungu amenisikiliza na amesikia sauti yangu katika maombi.
Sifa apewe Mungu, ambaye hakulikataa ombi langu wala kunizuilia upendo wake!
Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi. Wimbo. Mungu aturehemu na kutubariki, na kutuangazia nuru za uso wake,
ili njia zako zijulikane duniani, wokovu wako katikati ya mataifa yote.
Ee Mungu, mataifa na wakusifu, mataifa yote na wakusifu.
Mataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe, kwa kuwa unatawala watu kwa haki na kuongoza mataifa ya dunia.
Ee Mungu, mataifa na wakusifu, mataifa yote na wakusifu.
Ndipo nchi itatoa mazao yake, naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.
Mungu atatubariki na miisho yote ya dunia itamcha yeye.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.