Hesabu 34:16-29
16
Bwana akamwambia Mose,
17
“Haya ndiyo majina ya watu ambao watakusaidia kugawanya nchi kama urithi: Eleazari kuhani na Yoshua mwana wa Nuni.
18
Tena uteue kiongozi mmoja kutoka kila kabila kusaidia kuigawanya nchi.
19
Haya ndiyo majina yao: “Kalebu mwana wa Yefune, kutoka kabila la Yuda;
20
Shemueli mwana wa Amihudi, kutoka kabila la Simeoni;
21
Elidadi mwana wa Kisloni, kutoka kabila la Benyamini;
22
Buki mwana wa Yogli, kiongozi kutoka kabila la Dani;
23
Hanieli mwana wa Efodi, kiongozi kutoka kabila la Manase mwana wa Yosefu;
24
Kemueli mwana wa Shiftani, kiongozi kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yosefu;
25
Elisafani mwana wa Parnaki, kiongozi kutoka kabila la Zabuloni;
26
Paltieli mwana wa Azani, kiongozi kutoka kabila la Isakari;
27
Ahihudi mwana wa Shelomi, kiongozi kutoka kabila la Asheri;
28
Pedaheli mwana wa Amihudi, kiongozi kutoka kabila la Naftali.”
29
Hawa ndio watu ambao Bwana aliamuru wagawanye urithi kwa Waisraeli katika nchi ya Kanaani.
Settings