- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi80
Listen to this chapter
0:00
0:00
Mwito na Ombi la Kurejeshwa
1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Kuomboleza Hasira ya Mungu na Mateso ya Watu
4
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Israeli Kama Mzabibu Uliong’olewa
8
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Ombi Jipya la Mungu Kuingilia Kati
14
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note