Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Waiting Upon God: Should be done especially in adversity

10 mistari · 68 vipengele

Mistari kuhusu Should be done especially in adversity

  1. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.

  2. Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.

  3. Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.

  4. Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!

  5. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.

  6. Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.

  7. Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”

  8. Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.

  9. Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,

  10. Nitamngojea Bwana, ambaye ameificha nyumba ya Yakobo uso wake. Nitaliweka tumaini langu kwake.