Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu The Jews: Idolatry

12 mistari · 158 vipengele

Mistari kuhusu Idolatry

  1. Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.

  2. Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.

  3. Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.

  4. Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.

  5. Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.

  6. Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,

  7. makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.

  8. taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;

  9. watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,

  10. wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.

  11. “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:

  12. dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”