Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu The Jews: Under God's special protection

9 mistari · 158 vipengele

Mistari kuhusu Under God's special protection

  1. Mungu wa milele ni kimbilio lako, na chini kuna mikono ya milele. Atamfukuza adui yako mbele yako, akisema, ‘Mwangamize yeye!’

  2. Hivyo Israeli ataishi salama peke yake. Mzao wa Yakobo ni salama katika nchi ya nafaka na divai mpya, mahali ambapo mbingu hudondosha umande.

  3. Ee Israeli, wewe umebarikiwa! Ni nani kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana? Yeye ni ngao yako na msaada wako, na upanga wako uliotukuka. Adui zako watatetemeka mbele yako, nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.”

  4. walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

  5. Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:

  6. “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”

  7. Hatauacha mguu wako uteleze, yeye akulindaye hatasinzia,

  8. hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.

  9. Bwana anakulinda, Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,