Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Jewels

13 mistari · 7 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. Watu waliposikia habari hizo za huzuni, wakaanza kuomboleza wala hakuna mtu aliyevaa mapambo yoyote.

  2. Kwa kuwa Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni watu wenye shingo ngumu. Kama ningefuatana nanyi hata kwa muda mfupi, ningewaangamiza. Sasa vueni mapambo yenu, nami nitaamua nitakalowatendea.’ ”

  3. Hivyo Waisraeli wakavua mapambo yao katika Mlima wa Horebu.

  4. Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”

  5. Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.

  6. Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750

  7. Katika siku ile Bwana atawanyangʼanya uzuri wao: bangili, tepe za kichwani, mikufu yenye alama za mwezi mwandamo,

  8. vipuli, vikuku, shela,

  9. vilemba, mikufu ya vifundo vya miguu, mshipi, chupa za manukato na hirizi,

  10. pete zenye muhuri, pete za puani,

  11. Nikakupamba kwa vito: nikakuvika bangili mikononi mwako na mkufu shingoni mwako,

  12. nikaweka hazama puani mwako, vipuli masikioni mwako na taji nzuri sana kichwani mwako.

  13. Kwa hiyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha, nguo zako zilikuwa za kitani safi, hariri na nguo iliyokuwa imetariziwa. Chakula chako kilikuwa unga laini, asali na mafuta ya zeituni. Ukawa mzuri sana ukainuka kuwa malkia.