Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Heart

30 mistari · 2 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.

  2. Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako.

  3. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.

  4. Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.

  5. Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.

  6. Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.

  7. Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.

  8. Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.

  9. Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?

  10. Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko.

  11. Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko, kama nikikaa pande za mbali za bahari,

  12. hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.

  13. Kama nikisema, “Hakika giza litanificha na nuru inayonizunguka iwe usiku,”

  14. hata giza halitakuwa giza kwako, usiku utangʼaa kama mchana, kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.

  15. Moyo wenye furaha hufanya uso uchangamke, bali maumivu ya moyoni huponda roho.

  16. Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hujilisha upumbavu.

  17. Siku zote za wanaoonewa ni za taabu, bali moyo mchangamfu una karamu ya kudumu.

  18. Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, ni mwovu kupita kiasi. Ni nani awezaye kuujua?

  19. “Mimi Bwana huchunguza moyo na kuzijaribu nia, ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake, kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”

  20. Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.

  21. Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.

  22. Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”

  23. Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi, nitawatakasa kutoka uchafu wenu wote na kutoka sanamu zenu zote.

  24. Nitawapa moyo mpya na kuweka roho mpya ndani yenu, nitaondoa ndani yenu moyo wenu wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.

  25. Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.