Ayubu 19:1-22
1
Ndipo Ayubu akajibu:
2
“Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, na kuniponda kwa maneno yenu?
3
Mara kumi hizi mmenishutumu; bila aibu mnanishambulia.
4
Kama ni kweli nimepotoka, kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.
5
Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,
6
basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, naye amekokota wavu wake kunizunguka.
7
“Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.
8
Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.
9
Amenivua heshima yangu, na kuniondolea taji kichwani pangu.
10
Amenibomoa kila upande hadi nimeisha; amelingʼoa tegemeo langu kama mti.
11
Hasira yake imewaka juu yangu; amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake.
12
Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu; yamenizingira, yamepiga kambi kulizunguka hema langu.
13
“Amewatenga ndugu zangu mbali nami; wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa.
14
Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali; rafiki zangu wamenisahau.
15
Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni; wananitazama kama mgeni.
16
Namwita mtumishi wangu, wala haitiki, ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe.
17
Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu; nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe.
18
Hata watoto wadogo hunidhihaki; ninapojitokeza, hunifanyia mzaha.
19
Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa; wale niwapendao wamekuwa kinyume nami.
20
Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu; nimeponea nikiwa karibu kufa.
21
“Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.
22
Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo? Hamtosheki kamwe na mwili wangu?
Settings