Ayubu 18:15-21
15
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
16
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
17
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
18
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
19
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
20
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
21
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Settings