Ayubu 19:1-6
1
Ndipo Ayubu akajibu:
2
“Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, na kuniponda kwa maneno yenu?
3
Mara kumi hizi mmenishutumu; bila aibu mnanishambulia.
4
Kama ni kweli nimepotoka, kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.
5
Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,
6
basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, naye amekokota wavu wake kunizunguka.
Settings