Ayubu 19:7-12
7
“Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.
8
Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.
9
Amenivua heshima yangu, na kuniondolea taji kichwani pangu.
10
Amenibomoa kila upande hadi nimeisha; amelingʼoa tegemeo langu kama mti.
11
Hasira yake imewaka juu yangu; amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake.
12
Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu; yamenizingira, yamepiga kambi kulizunguka hema langu.
Settings