Ayubu 18:11-14
11
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14
Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
Settings