- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Ayubu8
Listen to this chapter
0:00
0:00
Bildadi amshutumu Ayubu na kuitetea haki ya Mungu
1
Kisha Bildadi Mshuhi akajibu:
2
“Hata lini wewe utasema mambo kama haya? Maneno yako ni kama upepo mkuu.
3
Je, Mungu hupotosha hukumu? Je, Mwenyezi hupotosha kile kilicho haki?
4
Watoto wako walipomtenda dhambi, aliwapa adhabu ya dhambi yao.
5
Lakini ukimtafuta Mungu, nawe ukamsihi Mwenyezi,
6
ikiwa wewe ni safi na mnyofu, hata sasa atainuka mwenyewe kwa niaba yako, na kukurudisha katika mahali pako pa haki.
7
Ijapokuwa mwanzo wako ulikuwa mdogo, lakini mwisho wako utakuwa wa mafanikio.
Mamlaka ya hekima ya kale
8
“Ukaulize vizazi vilivyotangulia na uone baba zao walijifunza nini,
9
kwa kuwa sisi tumezaliwa jana tu na hatujui lolote, nazo siku zetu duniani ni kama kivuli tu.
10
Je, hawatakufundisha na kukueleza? Je, hawataleta maneno kutoka kwenye kufahamu kwao?
Tumaini la waovu ladumu kwa muda mfupi
11
Je, mafunjo yaweza kumea mahali pasipo na matope? Matete yaweza kustawi bila maji?
12
Wakati bado yanaendelea kukua kabla ya kukatwa, hunyauka haraka kuliko majani mengine.
13
Huu ndio mwisho wa watu wote wanaomsahau Mungu; vivyo hivyo matumaini ya wasiomjali Mungu huangamia.
14
Lile analolitumainia huvunjika upesi; lile analolitegemea ni utando wa buibui.
15
Huutegemea utando wake, lakini hausimami; huungʼangʼania, lakini haudumu.
16
Yeye ni kama mti ulionyeshewa vizuri wakati wa jua, ukieneza machipukizi yake bustanini;
17
huifunganisha mizizi yake kwenye lundo la mawe, na kutafuta nafasi katikati ya mawe.
18
Unapongʼolewa kutoka mahali pake, ndipo mahali pale huukana na kusema, ‘Mimi kamwe sikukuona.’
19
Hakika uhai wake hunyauka, na kutoka udongoni mimea mingine huota.
Mungu atawarudisha wenye haki
20
“Hakika Mungu hamkatai mtu asiye na hatia, wala kuitia nguvu mikono ya mtenda mabaya.
21
Bado atakijaza kinywa chako na kicheko, na midomo yako na kelele za shangwe.
22
Adui zako watavikwa aibu, nazo hema za waovu hazitakuwepo tena.”
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note