Rukia maudhui

circa 1446–1406 BC

The Wilderness Years

Forty years of wandering in the desert test Israel's faith and prepare a new generation to enter the promised land.

2,247 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Kumbukumbu 28:19takriban 1451 KK

    Utalaaniwa uingiapo na utokapo.

  2. Kumbukumbu 28:20takriban 1451 KK

    Bwana ataleta laana juu yako, fadhaa na kukaripiwa katika kila kitu unachokigusa kwa mkono wako, mpaka uwe umeharibiwa na kuangamizwa ghafula kwa ajili ya maovu uliyoyafanya kwa kumwacha yeye.

  3. Kumbukumbu 28:21takriban 1451 KK

    Bwana atakupiga kwa magonjwa mpaka akuangamize kutoka nchi unayoingia kuimiliki.

  4. Kumbukumbu 28:22takriban 1451 KK

    Bwana atakupiga kwa magonjwa ya kudhoofisha, kwa homa na kuwashwa, hari na kwa ukame, kutu na kuwa na uchungu ambavyo vitakupiga mpaka uangamie.

  5. Kumbukumbu 28:23takriban 1451 KK

    Anga juu yako itakuwa shaba, na ardhi chini yako itakuwa chuma.

  6. Kumbukumbu 28:24takriban 1451 KK

    Bwana atafanya mvua ya nchi yako kuwa mavumbi na mchanga; vitakujia kutoka angani mpaka uangamie.

  7. Kumbukumbu 28:25takriban 1451 KK

    Bwana atakufanya ushindwe mbele ya adui zako. Utawajia kwa njia moja lakini utawakimbia mbele yao kwa njia saba, nawe utakuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia.

  8. Kumbukumbu 28:26takriban 1451 KK

    Mizoga yenu itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo mtu yeyote wa kuwafukuza.

  9. Kumbukumbu 28:27takriban 1451 KK

    Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri na kwa vidonda vitokavyo usaha na kuwashwa, ambako huwezi kuponywa.

  10. Kumbukumbu 28:28takriban 1451 KK

    Bwana atakupiga kwa wazimu, upofu na kuchanganyikiwa kwa akili.

  11. Kumbukumbu 28:29takriban 1451 KK

    Wakati wa adhuhuri utapapasapapasa huku na huko kama mtu kipofu katika giza. Hutafanikiwa katika lolote ufanyalo; siku baada ya siku utaonewa na kunyangʼanywa, wala hakuna yeyote atakayekuokoa.

  12. Kumbukumbu 28:30takriban 1451 KK

    Utaposa mke, lakini mtu mwingine atakutana naye kimwili. Utajenga nyumba, lakini hutaishi ndani yake. Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutakula matunda yake.

  13. Kumbukumbu 28:31takriban 1451 KK

    Ngʼombe wako atachinjwa mbele ya macho yako lakini hutakula nyama yake. Punda wako atachukuliwa kwa nguvu kutoka kwako wala hatarudishwa. Kondoo wako watapewa adui zako, wala hakuna mtu yeyote wa kuwaokoa.

  14. Kumbukumbu 28:32takriban 1451 KK

    Wanao na binti zako watatolewa kwa mataifa mengine, nawe utayachosha macho yako ukiwatazamia siku baada ya siku, hutakuwa na nguvu kuinua mkono.

  15. Kumbukumbu 28:33takriban 1451 KK

    Taifa usilolijua watakula mazao ya nchi yako na taabu ya kazi yako, hutakuwa na chochote, bali kuonewa kikatili siku zako zote.

  16. Kumbukumbu 28:34takriban 1451 KK

    Vitu utakavyoviona kwa macho yako vitakufanya wazimu.

  17. Kumbukumbu 28:35takriban 1451 KK

    Bwana atayapiga magoti yako na miguu yako kwa majipu yenye maumivu makali yasiyoponyeka, yakienea kutoka nyayo za miguu yako hadi utosini.

  18. Kumbukumbu 28:36takriban 1451 KK

    Bwana atakupeleka wewe na mfalme uliyemweka juu yako uende kwenye taifa ambalo hukulijua wewe wala baba zako. Huko utaabudu miungu mingine, miungu ya miti na mawe.

  19. Kumbukumbu 28:37takriban 1451 KK

    Utakuwa kitu cha kuchukiza, tena kitu cha kudharauliwa na kudhihakiwa kwa mataifa yote huko Bwana atakakokupeleka.

  20. Kumbukumbu 28:38takriban 1451 KK

    Utapanda mbegu nyingi katika shamba lakini utavuna haba, kwa sababu nzige watazila.

  21. Kumbukumbu 28:39takriban 1451 KK

    Utapanda mashamba ya mizabibu na kuyapalilia, lakini hutakunywa divai yake wala hutakusanya zabibu, kwa sababu wadudu watazila.

  22. Kumbukumbu 28:40takriban 1451 KK

    Utakuwa na mizeituni katika nchi yako yote, lakini hutatumia hayo mafuta yake, kwa sababu zeituni zitapukutika.

  23. Kumbukumbu 28:41takriban 1451 KK

    Utakuwa na wana na binti lakini hawatakuwa nawe, kwa sababu watachukuliwa mateka.

  24. Kumbukumbu 28:42takriban 1451 KK

    Makundi ya nzige yatavamia miti yako yote na mazao ya nchi yako.

  25. Kumbukumbu 28:43takriban 1451 KK

    Mgeni anayeishi miongoni mwako atainuka juu zaidi na zaidi kuliko wewe, lakini wewe utashuka chini zaidi na zaidi.