Rukia maudhui

circa 800–400 BC

The Hebrew Prophets

God speaks through Isaiah, Jeremiah, and the minor prophets—calling Israel to repentance and foretelling the coming Messiah.

3,706 mistari · 14 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Lakini upanga utatuliaje wakati Bwana ameuamuru, wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni pamoja na pwani yake?”

  2. Yeremia 48:1takriban 584 KK

    Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.

  3. Yeremia 48:2takriban 584 KK

    Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.

  4. Yeremia 48:3takriban 584 KK

    Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.

  5. Yeremia 48:4takriban 584 KK

    Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.

  6. Yeremia 48:5takriban 584 KK

    Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.

  7. Yeremia 48:6takriban 584 KK

    Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.

  8. Yeremia 48:7takriban 584 KK

    Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.

  9. Yeremia 48:8takriban 584 KK

    Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.

  10. Yeremia 48:9takriban 584 KK

    Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.

  11. Yeremia 48:10takriban 584 KK

    “Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!

  12. Yeremia 48:11takriban 584 KK

    “Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.

  13. Yeremia 48:12takriban 584 KK

    Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.

  14. Yeremia 48:13takriban 584 KK

    Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.

  15. Yeremia 48:14takriban 584 KK

    “Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?

  16. Yeremia 48:15takriban 584 KK

    Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.

  17. Yeremia 48:16takriban 584 KK

    “Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.

  18. Yeremia 48:17takriban 584 KK

    Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’

  19. Yeremia 48:18takriban 584 KK

    “Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.

  20. Yeremia 48:19takriban 584 KK

    Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’

  21. Yeremia 48:20takriban 584 KK

    Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.

  22. Yeremia 48:21takriban 584 KK

    Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,

  23. Yeremia 48:22takriban 584 KK

    katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,

  24. Yeremia 48:23takriban 584 KK

    katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,

  25. Yeremia 48:24takriban 584 KK

    katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.