Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Punishment: Delayed punishment

16 mistari · 2 vipengele

Mistari kuhusu Delayed punishment

  1. Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.

  2. Mungu anayemiliki milele, atawasikia na kuwaadhibu, watu ambao hawabadilishi njia zao, wala hawana hofu ya Mungu.

  3. Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,

  4. kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,

  5. mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:

  6. wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.

  7. “Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.

  8. Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,

  9. kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,

  10. watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.

  11. Wakati hukumu juu ya tendo ovu haitekelezwi upesi, mioyo ya watu hujaa mipango ya kutenda maovu.

  12. Ingawa mtu mwovu hufanya maovu mia moja na akaendelea kuishi maisha marefu, najua kwamba itakuwa bora zaidi kwa watu wanaomwogopa Mungu, wamchao Mungu.

  13. Lakini kwa sababu waovu hawamwogopi Mungu, hawatafanikiwa, maisha yao hayatarefuka kama kivuli.

  14. Ee Bwana, hata lini nitakuomba msaada, lakini wewe husikilizi? Au kukulilia, “Udhalimu!” Lakini hutaki kuokoa?

  15. Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma? Kwa nini unavumilia makosa? Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu; kuna mabishano na mapambano kwa wingi.

  16. Kwa hiyo sheria imepotoshwa, nayo haki haipo kabisa. Waovu wanawazunguka wenye haki, kwa hiyo haki imepotoshwa.