Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Phylactery

10 mistari · 2 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.

  2. Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”

  3. Sikia, ee Israeli: Bwana Mungu wako, Bwana ni mmoja.

  4. Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.

  5. Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako.

  6. Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo.

  7. Zifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako.

  8. Ziandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.

  9. Yawekeni haya maneno yangu katika mioyo yenu na akili zenu, yafungeni kama alama juu ya mikono yenu na kwenye paji za nyuso zenu.

  10. “Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao.