- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Philosophy
Mistari muhimu ya Biblia
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
“Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako: