Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Lasciviousness

68 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,

  2. aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.

  3. Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.

  4. Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba hudondoza asali, na maneno ya kinywa chake ni laini kuliko mafuta;

  5. lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo, mkali kama upanga ukatao kuwili.

  6. Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo; hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.

  7. Njia zenu ziwe mbali naye, msiende karibu na mlango wa nyumba yake,

  8. usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine na miaka yako kwa aliye mkatili,

  9. wageni wasije wakasherehekea utajiri wako na jitihada yako ikatajirisha nyumba ya mwanaume mwingine.

  10. Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu, wakati nyama na mwili wako vimechakaa.

  11. Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!

  12. Sikuwatii walimu wangu wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.

  13. Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.

  14. Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.

  15. Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke

  16. wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.

  17. Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.

  18. (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;

  19. mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)

  20. Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:

  21. “Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.

  22. Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!

  23. Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.

  24. Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.

  25. Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!