God
Mistari inayomtaja God
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema; Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
Jifurahishe katika Bwana naye atakupa haja za moyo wako.
Mkabidhi Bwana njia yako, mtumaini yeye, naye atatenda hili:
Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko, na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.
Tulia mbele za Bwana na umngojee kwa uvumilivu; usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao, wanapotekeleza mipango yao miovu.
Kwa maana waovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi.
bali Bwana huwacheka waovu, kwa sababu anajua siku yao inakuja.
kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa, lakini Bwana humtegemeza mwenye haki.
Bwana anazifahamu siku za wanyofu, na urithi wao utadumu milele.
Lakini waovu wataangamia: Adui za Bwana watakuwa kama uzuri wa mashamba, watatoweka, watatoweka kama moshi.
Wale wanaobarikiwa na Bwana watairithi nchi, bali wale anaowalaani watakatiliwa mbali.
Kama Bwana akipendezwa na njia ya mtu, yeye huimarisha hatua zake,
ajapojikwaa, hataanguka, kwa maana Bwana humtegemeza kwa mkono wake.
Kwa kuwa Bwana huwapenda wenye haki naye hatawaacha waaminifu wake. Watalindwa milele, lakini uzao wa waovu utakatiliwa mbali.
Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; nyayo zake hazitelezi.
lakini Bwana hatawaacha mikononi mwao wala hatawaacha wahukumiwe kuwa wakosa wanaposhtakiwa.
Mngojee Bwana, na uishike njia yake. Naye atakutukuza uirithi nchi, waovu watakapokatiliwa mbali, utaliona hilo.
Wokovu wa wenye haki hutoka kwa Bwana, yeye ni ngome yao wakati wa shida.
Bwana huwasaidia na kuwaokoa, huwaokoa kutoka kwa waovu na kuwahifadhi, kwa maana wanamkimbilia.
Zaburi ya Daudi. Maombi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.
Kwa kuwa mishale yako imenichoma, na mkono wako umenishukia.
Hakuna afya mwilini mwangu kwa sababu ya ghadhabu yako, mifupa yangu haina uzima kwa sababu ya dhambi zangu.