Zaburi 69:7-21
7
Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako, aibu imefunika uso wangu.
8
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.
9
Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila, matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.
10
Ninapolia na kufunga, lazima nivumilie matusi.
11
Ninapovaa nguo ya gunia, watu hunidharau.
12
Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga, nimekuwa wimbo wa walevi.
13
Lakini Ee Bwana, ninakuomba, kwa wakati ukupendezao; katika upendo wako mkuu, Ee Mungu, unijibu kwa wokovu wako wa hakika.
14
Uniokoe katika matope, usiniache nizame; niokoe na hao wanichukiao, kutoka kwenye vilindi vya maji.
15
Usiache mafuriko yanigharikishe au vilindi vinimeze, au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.
16
Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako; kwa huruma zako nyingi unigeukie.
17
Usimfiche mtumishi wako uso wako, uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.
18
Njoo karibu uniokoe, nikomboe kwa sababu ya adui zangu.
19
Unajua jinsi ninavyodharauliwa, kufedheheshwa na kuaibishwa, adui zangu wote unawajua.
20
Dharau zimenivunja moyo na nimekata tamaa, nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata, wa kunituliza, lakini sikumpata.
21
Waliweka nyongo katika chakula changu na walinipa siki nilipokuwa na kiu.
Settings