Rukia maudhui
Mithali 30:1-6

Maneno ya Aguri: Utangulizi

Mithali 30:1-6
1
Misemo ya Aguri mwana wa Yake, usia: Huyu mtu alimwambia Ithieli, naam, kwa Ithieli na kwa Ukali:
2
“Mimi ni mjinga kuliko wanadamu wote; sina ufahamu wa kibinadamu.
3
Sijajifunza hekima, wala sina maarifa ya kumjua yeye Aliye Mtakatifu.
4
Ni nani ameshapanda mbinguni na kushuka? Ni nani ameshakusanya upepo kwenye vitanga vya mikono yake? Ni nani ameshafungia maji kwenye nguo yake? Ni nani ameimarisha miisho yote ya dunia? Jina lake ni nani, na mwanawe anaitwa nani? Niambie kama unajua!
5
“Kila neno la Mungu ni kamilifu; yeye ni ngao kwa wale wanaomkimbilia.
6
Usiongeze kwenye maneno yake, ama atakukemea na kukuthibitisha kuwa mwongo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options