Sala ya Aguri ya Kiasi
7
“Ninakuomba vitu viwili, Ee Bwana; usininyime kabla sijafa:
8
Uutenge mbali nami udanganyifu na uongo; usinipe umaskini wala utajiri, bali unipe chakula cha kunitosha kila siku.
9
Nisije nikawa na vingi vya kuzidi nikakukana na kusema, ‘Bwana ni nani?’ Au nisije nikawa maskini nikaiba, nami nikaliaibisha jina la Mungu wangu.
10
“Usimchongee mtumishi kwa bwana wake, asije akakulaani, ukapatilizwa kwalo.
Settings