Vizazi Vinne vya Waovu
11
“Wako watu wale ambao huwalaani baba zao na wala hawawabariki mama zao;
12
wale ambao ni safi machoni pao wenyewe kumbe hawakuoshwa uchafu wao;
13
wale ambao daima macho yao ni ya kiburi, ambao kutazama kwao ni kwa dharau;
14
wale ambao meno yao ni panga na ambao mataya yao yamewekwa visu kuwaangamiza maskini katika nchi, na wahitaji kutoka miongoni mwa wanadamu.
Settings