Rukia maudhui
Yoshua 19:32-39

Urithi wa Naftali

Yoshua 19:32-39
32
Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
33
Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34
Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35
Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
36
Adama, Rama, Hazori,
37
Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38
Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39
Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options