Rukia maudhui
Ayubu 30:9-15

Kudhihakiwa na kutendwa vibaya

Ayubu 30:9-15
9
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options