Skip to content
Mwanzo 10:6-20

Mwanzo 10:6-20

6
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17
Wahivi, Waariki, Wasini,
18
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options