Rukia maudhui

Zaburi61

Sala ya Kimbilio Wakati wa Taabu

1
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za uimbaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, sikia kilio changu, usikilize maombi yangu.
2
Kutoka miisho ya dunia ninakuita, ninaita huku moyo wangu unadhoofika; uniongoze kwenye mwamba ule ulio juu kuliko mimi.
3
Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.
4
Natamani kukaa hemani mwako milele, na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.

Uhakika katika Agano la Milele la Mungu

5
Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu, umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.
6
Mwongezee mfalme siku za maisha yake, miaka yake kwa vizazi vingi.
7
Yeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi mbele za Mungu milele; amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.

Nadhiri ya Sifa ya Kudumu

8
Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options