- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi49
Listen to this chapter
0:00
0:00
Mwito wa Wote Kusikia Hekima
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Sikieni haya, enyi mataifa yote, sikilizeni, ninyi wote mkaao dunia hii.
2
Wakubwa kwa wadogo, matajiri na maskini pamoja:
3
Kinywa changu kitasema maneno ya hekima, usemi wa moyo wangu utatoa ufahamu.
4
Nitatega sikio langu nisikilize mithali, nitafafanua kitendawili kwa zeze:
Upumbavu wa Kutumaini Utajiri
5
Kwa nini niogope siku mbaya zinapokuja, wakati wadanganyifu waovu wanaponizunguka,
6
wale wanaotegemea mali zao na kujivunia utajiri wao mwingi?
7
Hakuna mwanadamu awaye yote awezaye kuukomboa uhai wa mwingine, au kumpa Mungu fidia kwa ajili yake.
8
Fidia ya uhai ni gharama kubwa, hakuna malipo yoyote yanayotosha,
9
ili kwamba aishi milele na asione uharibifu.
10
Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia na kuwaachia wengine mali zao.
11
Makaburi yao yatabaki kuwa nyumba zao za milele, makao yao vizazi vyote; ingawa walikuwa na mashamba na kuyaita kwa majina yao.
12
Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu; anafanana na mnyama aangamiaye.
Kaburi Linamngojea Mpumbavu Tajiri
13
Hii ndiyo hatima ya wale wanaojitumainia wenyewe, pia ya wafuasi wao, waliothibitisha misemo yao.
14
Kama kondoo, wamewekewa kwenda kaburini, nacho kifo kitawala. Wanyofu watawatawala asubuhi, maumbile yao yataozea kaburini, mbali na majumba yao makubwa ya fahari.
15
Lakini Mungu atakomboa uhai wangu na kaburi, hakika atanichukua kwake.
Usiwaonee Wivu Wanaofanikiwa Duniani
16
Usitishwe mtu anapotajirika, fahari ya nyumba yake inapoongezeka,
17
kwa maana hatachukua chochote atakapokufa, fahari yake haitashuka pamoja naye.
18
Ingawa alipokuwa akiishi alijihesabu kuwa heri, na wanadamu wanakusifu unapofanikiwa,
19
atajiunga na kizazi cha baba zake, ambao hawataona kamwe nuru ya uzima.
20
Mwanadamu mwenye utajiri bila ufahamu ni kama wanyama waangamiao.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note