Rukia maudhui

Zaburi130

Kilio Kutoka Vilindini

1
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.

Msamaha Ndio Msingi wa Tumaini

3
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.

Kumngojea Mungu kwa Saburi

5
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.

Tumaini na Ukombozi kwa Israeli

7
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options