- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mithali18
Listen to this chapter
0:00
0:00
Kutafuta Hekima na Haki
1
Mtu ajitengaye na wengine hufuata matakwa yake mwenyewe; hupiga vita kila shauri jema.
2
Mpumbavu hafurahii ufahamu, bali hufurahia kutangaza maoni yake mwenyewe.
3
Wakati uovu unapokuja, dharau huja pia, pamoja na aibu huja lawama.
4
Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kina cha maji, bali chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
5
Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu, au kumnyima haki asiye na hatia.
Hatari ya Maneno ya Mpumbavu na Uvivu
6
Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi na kinywa chake hualika kipigo.
7
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na midomo yake ni mtego kwa nafsi yake.
8
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
9
Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu.
Usalama wa Kweli na wa Uongo
10
Jina la Bwana ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama.
11
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, wanaudhania kuwa ukuta usioweza kurukwa.
12
Kabla ya anguko moyo wa mtu hujaa kiburi, bali unyenyekevu hutangulia heshima.
Hekima Katika Hukumu na Nguvu ya Ndani
13
Yeye ajibuye kabla ya kusikiliza, huo ni upumbavu wake na aibu yake.
14
Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili?
15
Moyo wa mwenye ufahamu hujipatia maarifa, masikio ya mwenye hekima huyatafuta maarifa.
16
Zawadi humfungulia njia mtoaji, nayo humleta mbele ya wakuu.
17
Yeye aliye wa kwanza kuleta mashtaka huonekana sahihi, hadi mwingine ajitokezapo na kumuuliza maswali.
18
Kupiga kura hukomesha mashindano na kutenganisha wapinzani wakuu wanaopingana.
Mahusiano na Nguvu ya Ulimi
19
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuridhika kuliko mji uliozungushiwa ngome, nayo mabishano ni kama malango ya ngome yenye makomeo.
20
Tumbo la mtu litajaa kutokana na tunda la kinywa chake, atashibishwa mavuno yanayotokana na midomo yake.
21
Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi, nao waupendao watakula matunda yake.
Ndoa na Urafiki
22
Apataye mke apata kitu chema naye ajipatia kibali kwa Bwana.
23
Mtu maskini huomba kuhurumiwa bali tajiri hujibu kwa ukali.
24
Mtu mwenye marafiki wengi wanaweza kumharibu, bali yuko rafiki aambatanaye na mtu kwa karibu kuliko ndugu.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note