- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Ayubu23
Listen to this chapter
0:00
0:00
Ayubu atamani kutetea shauri lake mbele za Mungu
1
Ndipo Ayubu akajibu:
2
“Hata leo malalamiko yangu ni chungu; mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.
3
Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
4
Ningeliweka shauri langu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
5
Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile ambalo angelisema.
6
Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, asingenigandamiza.
7
Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
Mungu amefichika, lakini Ayubu adumu mwaminifu
8
“Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
9
Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
10
Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
11
Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; nimeishika njia yake bila kukengeuka.
12
Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake; nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.
Enzi kuu ya Mungu isiyobadilika
13
“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? Yeye hufanya lolote atakalo.
14
Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.
15
Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; nifikiriapo haya yote ninamwogopa.
16
Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; yeye Mwenyezi amenitia hofu.
17
Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note