Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Wife: Procured

8 mistari · 13 vipengele

Mistari kuhusu Procured

  1. Shekemu akamwambia baba yake Hamori, “Nipatie msichana huyu awe mke wangu.”

  2. Yakobo aliposikia kwamba binti yake Dina amenajisiwa, wanawe walikuwa mashambani wakichunga mifugo yake, kwa hiyo akalinyamazia jambo hilo mpaka waliporudi nyumbani.

  3. Kisha Hamori baba yake Shekemu akaenda kuzungumza na Yakobo.

  4. Basi wana wa Yakobo walikuwa wamerudi kutoka mashambani mara tu waliposikia kilichotokea. Walikuwa wamejawa na huzuni na ghadhabu, kwa sababu Shekemu alikuwa amefanya jambo la aibu katika Israeli kwa kukutana kimwili na binti wa Yakobo, kitu ambacho hakingepasa kufanyika.

  5. Lakini Hamori akawaambia, “Moyo wa mwanangu Shekemu umeelekea kwa binti yenu. Tafadhali mpeni awe mke wake.

  6. Oaneni na sisi, tupeni binti zenu, nanyi mchukue binti zetu.

  7. Mwaweza kuishi katikati yetu, nchi ni wazi kwenu. Ishini ndani yake, fanyeni biashara humu na mjipatie mali.”

  8. Yuda akampatia Eri, mzaliwa wake wa kwanza, mke aitwaye Tamari.