Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Pawn

13 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. Kama ukichukua vazi la jirani kama rehani, ulirudishe kwake kabla jua kuzama,

  2. Unapomkopesha jirani yako chochote, usiingie nyumbani kwake kutwaa kile anachokitoa kama rehani.

  3. Ukae nje na umwache huyo mtu uliyemkopesha akuletee hiyo rehani.

  4. Ikiwa mtu huyo ni maskini, usiende kulala ukiwa na hiyo rehani yake katika milki yako.

  5. Rudisha vazi lake kabla ya machweo ya jua ili apate kulilalia. Kisha atakushukuru na kitaonekana kama kitendo cha haki mbele za Bwana Mungu wako.

  6. Usipotoshe hukumu ya mgeni au yatima, au kuchukua vazi la mjane kama rehani.

  7. Huwanyangʼanya yatima punda wao, na kumchukua rehani fahali wa mjane.

  8. Kama ukikosa njia ya kulipa, kitanda chako kitachukuliwa ukiwa umekilalia.

  9. “Mtu aweza kuwa ni mwenye haki atendaye yaliyo haki na sawa.

  10. Hamwonei mtu yeyote, bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.

  11. Huwaonea maskini na wahitaji. Hunyangʼanyana. Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake. Huziinulia sanamu macho. Hufanya mambo ya machukizo.

  12. kama akirudisha kile alichochukua rehani kwa ajili ya deni, akarudisha alichoiba na kufuata amri zile ziletazo uzima, wala hafanyi uovu, hakika ataishi, hatakufa.

  13. Watu hulala kando ya kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani. Katika nyumba ya mungu wao hunywa mvinyo ulionunuliwa kwa fedha walizotozwa watu.