Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Love to Man: Visiting the sick, &c

7 mistari · 73 vipengele

Mistari kuhusu Visiting the sick, &c

  1. “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,

  2. kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;

  3. lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:

  4. kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi

  5. ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,

  6. na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,

  7. basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.