Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Christ is God

56 mistari · 55 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.

  2. Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako.

  3. Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”

  4. Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.

  5. Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.

  6. Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”