Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Abomination

20 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. Haimpasi mwanamke kuvaa nguo za kiume wala mwanaume kuvaa nguo za kike, kwa maana Bwana Mungu wenu anachukia yeyote ambaye hufanya hivi.

  2. kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.

  3. Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:

  4. macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

  5. moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,

  6. shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.

  7. Kinywa changu husema lililo kweli, kwa maana midomo yangu huchukia uovu.

  8. Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.

  9. Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.

  10. Bwana huchukia sana dhabihu za waovu, bali maombi ya wanyofu humfurahisha Mungu.

  11. Bwana huchukia sana njia ya waovu, bali huwapenda wale wafuatao haki.

  12. Bwana huchukia sana mawazo ya mwovu, bali mawazo ya wale walio safi humfurahisha yeye.

  13. Bwana huwachukia sana wote wenye kiburi cha moyo. Uwe na hakika kwa hili: Hawataepuka kuadhibiwa.

  14. Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.

  15. Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.

  16. Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.

  17. Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!

  18. Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.

  19. Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.

  20. Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.