God
Mistari inayomtaja God
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake, wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa, waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Lishangilieni jina lake takatifu, mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Mtafuteni Bwana na nguvu zake, utafuteni uso wake siku zote.
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu, hukumu zake zimo duniani pote.
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,