God
Mistari inayomtaja God
Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato. Ni vyema kumshukuru Bwana na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
kuutangaza upendo wako asubuhi, na uaminifu wako wakati wa usiku,
Ee Bwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha, nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako.
Ee Bwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako, tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!
Bali wewe, Ee Bwana, utatukuzwa milele.
Ee Bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.
Umeitukuza pembe yangu kama ile ya nyati dume, mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.
waliopandwa katika nyumba ya Bwana, watastawi katika nyua za Mungu wetu.
wakitangaza, “Bwana ni mkamilifu; yeye ni Mwamba wangu, na ndani yake hamna uovu.”
Bwana anatawala, amejivika utukufu; Bwana amejivika utukufu tena amejivika nguvu. Dunia imewekwa imara, haitaondoshwa.
Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani; wewe umekuwako tangu milele.
Bahari zimeinua, Ee Bwana, bahari zimeinua sauti zake; bahari zimeinua sauti za mawimbi yake.
Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu, ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari: Bwana aishiye juu sana ni mkuu.
Ee Bwana, sheria zako ni imara; utakatifu umepamba nyumba yako pasipo mwisho.
Ee Bwana, ulipizaye kisasi, Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.
Ee Mhukumu wa dunia, inuka, uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.
Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
Je, aliyeweka sikio asisikie? Aliyeumba jicho asione?
Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?
Bwana anajua mawazo ya mwanadamu; anajua kwamba ni ubatili.
Ee Bwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, mtu unayemfundisha kwa sheria yako,