Rukia maudhui
Wimbo 6:4-10

Bwana-arusi Asifu Uzuri wa Bibi-arusi

Wimbo 6:4-10
4
Wewe ni mzuri, mpenzi wangu, kama Tirsa, upendezaye kama Yerusalemu, umetukuka kama jeshi lenye bendera.
5
Uyageuze macho yako mbali nami, yananigharikisha. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi wanaoteremka kutoka Gileadi.
6
Meno yako ni kama kundi la kondoo watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye peke yake.
7
Mashavu yako nyuma ya shela yako ni kama vipande viwili vya komamanga.
8
Panaweza kuwepo malkia sitini, masuria themanini na mabikira wasiohesabika;
9
lakini hua wangu, mkamilifu wangu, ni wa namna ya pekee, binti pekee kwa mama yake, kipenzi cha yeye aliyemzaa. Wanawali walimwona na kumwita aliyebarikiwa; malkia na masuria walimsifu.
10
Ni nani huyu atokeaye kama mapambazuko, mzuri kama mwezi, mwangavu kama jua, ametukuka kama nyota zifuatanazo?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options