Rukia maudhui
Luka 22:39-46

Yesu Asali katika Mlima wa Mizeituni

Luka 22:39-46
39
Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata.
40
Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.”
41
Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba
42
akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.”
43
Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu.
44
Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.
45
Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni.
46
Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options