Ayubu 29:1-11
1
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
Settings